Monday, 27 April 2015

Nimekuletea Simu mpya Huawei P8 uiangalie

Huawei P8max
MORE PICTURES
  • 7.4%POPULARITY
  • 7.7DESIGN
  • 7.4FEATURES
  • 7.7PERFORMANCE

NETWORK
TechnologyGSM / HSPA / LTE
2G bandsGSM 850 / 900 / 1800 / 1900 - SIM 1 & SIM 2
3G bandsHSDPA 850 / 900 / 1900 / 2100
4G bandsLTE
 
 
 
SpeedHSPA 42.2/5.76 Mbps, LTE Cat6 300/50 Mbps
GPRSYes
EDGEYes
LAUNCH
Announced2015, April
StatusComing soon. Exp. release 2015, May
BODY
Dimensions182.7 x 93 x 6.8 mm (7.19 x 3.66 x 0.27 in)
Weight228 g (8.04 oz)
SIMDual SIM (Nano-SIM, dual stand-by)
DISPLAY
TypeLTPS LCD capacitive touchscreen, 16M colors
Size6.8 inches (~74.1% screen-to-body ratio)
Resolution1080 x 1920 pixels (~326 ppi pixel density)
MultitouchYes
ProtectionCorning Gorilla Glass 3
 - Emotion UI
PLATFORM
OSAndroid OS, v5.0.2 (Lollipop)
ChipsetHiSilicon Kirin 935
CPUQuad-core 2.2 GHz Cortex-A53 & quad-core 1.5 GHz Cortex-A53
GPUMali-T628 MP4
MEMORY
Card slotmicroSD, up to 64 GB (uses SIM 2 slot)
Internal64 GB, 3 GB RAM
CAMERA
Primary13 MP, 4160 x 3120 pixels, autofocus, optical image stabilization, dual-LED (dual tone) flash
FeaturesGeo-tagging, touch focus, face/smile detection, panorama, HDR
Video1080p@30fps
Secondary5 MP
SOUND
Alert typesVibration; MP3, WAV ringtones
LoudspeakerYes
3.5mm jackYes
COMMS
WLANWi-Fi 802.11 a/b/g/n, dual-band, Wi-Fi Direct, DLNA, hotspot
Bluetoothv4.0, A2DP
GPSYes, with A-GPS, GLONASS
NFCYes
RadioTBC
USBmicroUSB v2.0, USB Host
FEATURES
SensorsAccelerometer, gyro, proximity, compass
MessagingSMS(threaded view), MMS, Email, Push Mail, IM
BrowserHTML5
JavaNo
 - Active noise cancellation with dedicated mic
- XviD/MP4/H.264 player
- MP3/eAAC+/WAV/Flac player
- Document viewer
- Photo/video editor

BATTERY
 Non-removable Li-Po 4360 mAh battery

Saturday, 25 April 2015

Kampuni ya Google imatangaza kuwa itazindua huduma mpya nchini Marekani ambayo inaweza kutumiwa nyumbani na wakati wa safari za mataifa ya kigeni.


Huduma ya Project Fi
Huduma hiyo inayo fahamika kama Project Fi inatapatikana kwa simu za Smartphone za Google Nexus 6.
Huduma hiyo itatumia maeneo yaliyo na Wi-Fi sambamba na huduma zingine za mawasilianoi nchini Marekani za Sprint na T-Mobile na inaweza pia kutumiwa kwenye nchi 120 bila malipo ya ziada wakati mtu anaposafiri nje ya nchi.
Huduma hiyo itatolewa kwa malipo ya dola ishirini kwa mwezi kwa huduma za kawaida na dola kumi kwa mwezi kwa kila gigabyte ya data inayotumika.
Google inasema kuwa huduma hiyo huwa inajiunga moja kwa moja na zaidi maeneo milioni yenye huduna za Wi-Fi na mteja ana uwezo wa kuhamiswa kutoka kwa mtandao mmoja hadi mwingine kulingana na ni upi unaotoa huduma bora zaidi.

Monday, 20 April 2015

Tanzania kuwaondoa raia wake walioko Afrika Kusini


Serikali ya Tanzania imetangaza kuwa, inapanga kuwaondoa raia wake huku nchini Afrika Kusini baada ya kushadidi hujuma na mashambulio dhidi ya raia wa kigeni katika nchi hiyo. 

Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini umesema umeanza zoezi la kuwatambua Watanzania waishio katika maeneo ya hatari nchini humo kabla ya kuanza hatua za kuwaondoa na kuwarejesha nyumbani. 

Mkuu wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mindi Kasiga, amesema kwamba Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini umepeleka maofisa wake katika mji wa Durban kuangalia hali ilivyo. 

Kasiga ameongeza kuwa, serikali imeshatoa mwongozo wa namna ya kuwaondoa raia wake nchini Afrika Kusini. 

Aidha amesema, utaratibu wa kuwaondoa Watanzania upo tayari, lakini si kila Mtanzania anayeishi Afrika Kusini ataondolewa, bali wale walio katika maeneo hatari. 

Mamia ya raia wa kigeni wanaoishi Afrika Kusini wamekimbilia katika kambi zilizowekwa katika miji ya Johannesburg na Durban wakihofia maisha yao na hadi sasa raia sita wa kigeni wameshauawa katika hujuma hiyo. 

Mashambulizi hayo yalishika kasi zaidi baada ya Mfalme wa Zulu, Goodwill Zwelithini kaBhekuzulu, kunukuliwa na vyombo vya habari mwezi uliopita akisema kuwa raia wa nchi za Kigeni wanapaswa kuondoka nchini humo.

Thursday, 16 April 2015

ABU 5 AJALI YA BASI NA FUSO

Muonekano wa alama ya mnyama anayefanana na Chui akitembea akiwa na mtoto wakati wa magari hayo yakiwaka moto.
MAAJABU matano yameibuka kufuatia ajali mbaya iliyohusisha lori aina ya Fuso na basi la abiria iliyotokea Jumapili iliyopita eneo la Iyovi, Ruaha, Kilosa mkoani Morogoro ambapo zaidi ya watu 19 walifariki dunia, 13 kati yao kuteketea kwa moto na kuzikwa kwenye kaburi moja katika Makaburi ya Msavu mwanzoni mwa wiki hii.
Ajali hiyo ilitokea baada ya lori hilo lenye namba za usajili T 164 BKG kugongana na basi la abiria la Kampuni ya Nganga lenye namba za usajili T 373 DAH lililokuwa likisafiri kutoka Kilombero mkoani Morogoro kuelekea Mbeya eneo la Kijiji cha Msimba katika Tarafa ya Mikumi.
Picha ikionyesha mtu akiwa amevaa vazi la kanzu huku kiunoni kama  amejifunga mkanda, kama zilivyo picha za kuchorwa zinazowaonesha wanafunzi wa Yesu, Inasemwa na watu kuwa mtu huyo, huenda ni malaika wa amani.
Ajabu la kwanza linaloonekana kwenye picha zilizopigwa wakati magari hayo yakiungua moto, zinaonesha alama ya mnyama anayefanana na Chui akitembea akiwa na mtoto wake, kitu ambacho kimewafanya watu wengi kushindwa kutafsiri suala hilo.
Kana kwamba haitoshi, katika picha hiyo chini kidogo ya mnyama huyo, kuna ajabu lingine ambapo picha kama ya mtu akiwa amevaa vazi la kanzu huku kiunoni kama  amejifunga mkanda, kama zilivyo picha za kuchorwa zinazowaonesha wanafunzi wa Yesu. Inasemwa na watu kuwa mtu huyo, huenda ni malaika wa amani.
Ajabu la tatu katika tukio hilo la kusikitisha ni mpigapicha ambaye anahisiwa kuwa ndani ya gari dogo, umbali wa mita kadhaa kutoka eneo la tukio. Lakini wakati picha hiyo ikionesha mvua zilikuwa zikinyesha na barabara kuonekana kuloa kutokana na maji ya mvua, lakini katika eneo ambalo magari hayo yaligongana, kunaonekana kukavu jambo linalozua maswali mengi kuliko majibu.
Ajabu la nne ni kuwepo kwa taarifa kutoka kwa walionusurika katika ajali hiyo kuwa mmoja wa marehemu, aliweza kuzungumza kwa simu na wanaodhaniwa kuwa ndugu zake wakati akiteketea kwa moto. Inadaiwa kuwa walimsikia akiwaambia kuwa sauti wanayoisikia ni ya moto na kwamba atakata kauli wakati wowote na hakuelewa kama wangeitambua maiti yake.
Muonekano wa magari hayo baada ya kuwaka moto.
Na ajabu la mwisho kabisa katika ajali hiyo ni maelezo ya kuwa mmoja wa marehemu aliyefariki dunia baada ya kuungua moto, ni pale alipotambuliwa baada ya kuonekana mabaki ya mguu wake mmoja, uliokuwa na kiatu. Inadaiwa kuwa ndugu walimtambua kutokana na masalia ya kiatu hicho, ingawa mwili wake wote ulikuwa umeungua vibaya na asingeweza kutambuliwa.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili kuhusu ajali hiyo, mtabiri maarufu Maalim Yahya Hussein, alisema ajali hiyo haikuwa ya kawaida, kwani siyo rahisi kwa moto kuanzia kwenye buti, tena kwa mlipuko wa ghafla. Aliihusisha ajali hiyo na harakati za kisiasa, akisema ni mwaka wa uchaguzi, ambao una mambo mengi.
Polisi wakiwa eneo la tukio.
Kuhusu picha ya mtu anayeonekana, ambaye katika mitandao kadhaa ya kijamii anatajwa kuwa ni malaika, alisema anayeonekana siyo malaika, kwani wao kazi yao ni kusaidia.
Mazishi ya watu hao yalifanyika Jumatatu iliyopita na kuhudhuriwa na viongozi wa dini zote, wa serikali na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa, tukio hilo la simanzi lililowatoa machozi mamia ya waombolezaji waliojitokeza.


Chanzo paparazihuru